×
New Times Tanzania New Times Tanzania is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services.
New Times Tanzania

SERIKALI YATAHADHARI ONGEZEKO LA WAGONJWA WA UVIKO – 19

Na Mwandishi wetu.

Serikali kupitia Wizara ya Afya imeeleza kuwa tangu Mwezi Februari hadi Aprili Mwaka huu Kuna ongezeko la visa vya maambukizi ya ugonjwa Wa Uviko -19 nchini.

Amesema Takwimu zinaonyesha Katika kipindi hicho Kuna ongezeko la asimilia 1.4 ( wagonjwa 2 kati ya watu 139 waliopimwa), mwezi Februari hadi asilimia 16.3 (Wagonjwa 31 kati ya watu 190 waliopimwa) Mwezi Machi, na Kisha asilimia 16.8 ( Wagonjwa 31 kati ya Watu 185 waliopimwa) mwezi Aprili 2025.

Hayo yamewekwa wazi Katika taarifa yake Mganga Mkuu Wa Serikali Dkt. Grace Magembe amesema kuongezeka na kupungua Kwa Uviko-19 kumekuwepo Kila Mwaka tangu kutangazwa Kwa ugonjwa huo nchini Mwaka 2020.

#NTTUpdates