Na Mwandishi wetu.
Mabingwa mara nne mfululizo wa ligi kuu ya NBC Young Africans SC imemuongezea mkataba wa miaka miwili 2 kiungo wao Mudathir Yahaya Abbas hadi 2027 kuendelea kuwatumikia Mabingwa hao wa kihistoria.
Mudathir amekuwa na kiwango bora toka ajiunge na miamba hiyo ya mitaa ya Twiga na Jangwani na ataendelea kuwatumikia kwa misimu miwili tena.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na Young Africans SC 2023 baada ya kuachana na klabu yake ya Azam FC.
#NTTupdates